MAMBO KAMA YALIVYO NJE YA TANZANIA

Monday 16 April 2012

JACOB ZUMA KUOA TENA WIKIEND IJAYO

18:43 By Mindset

Picha na wikipedia

Raisi wa jamhuri ya Afrika ya Kusini, anatarajiwa kuoa tena wikiend ijayo, mara hii atakuwa anafikisha mke wa NNE.

Kwa mujibu wa habari nilizoshuhudia kwa vituo vya television vya hapa Sauzi, pia kujionea katika magazeti ya jana Jumapili, inadaiwa raisi Jacob Zuma atafunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu bi Bongi Ngema, ambaye kwa mujibu wa www.iol.co.za raisi Zuma na bi Bongi Ngema tayari wana mtoto wa miaka minne.

Kwa mujibu wa www.iol.co.za Msemaji wa raisi Mac Maharaj amewaondoa wananchi hofu kuwa raisi atatumia hela zake binafsi na hakuna hela ya mlipa kodi itakayotumika katika kufanikisha sherehe hiyo ya harusi ambayo itakuwa ni shughuli binafsi.

0 comments: