MAMBO KAMA YALIVYO NJE YA TANZANIA

Thursday 12 April 2012

GHANA WAJIPANGA KUCHUKUA KOMBE LA AFRIKA MWAKANI

10:52 By Mindset

Aliyekuwa nahodha wa timu ya taifa ya Ghana ,  Kwesi Appiah ameteuliwa kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya Ghana -Black Stars.

Kwa mujibu wa ghanaweb.com , Appiah amepewa ulaji wa mkataba wa miaka miwili na ana kibarua kizito cha kuhakikisha malengo ya taifa hilo katika soka yanafikiwa, malengo hayo ni kuhakikisha kuwa katika fainali ijayo ya dunia Ghana inafika Nusu fainali na katika fainali za kombe la mataifa ya Afrika, taifa hilo linabeba kombe hilo.

Haya kazi ndiyo hiyo, wenzetu wa Ghana wameweka malengo.  
Toa maoni yako, kwetu sisi wabongo, tuna malengo yapi na tumejipangaje kufikia malengo hayo kwa kombe la dunia na kombe la mataifa ya Afrika ?

0 comments: