MAMBO KAMA YALIVYO NJE YA TANZANIA

Thursday 1 March 2012

GOOGLE NA SERA MPYA: ZITAMBUE ZINAVYOATHIRI UHURU WAKO

17:47 By Mindset


Kuanzia leo Tarehe 1, Machi 2012 Google imeanza kutumia sera yake mpya inayoruhusu kufuatilia taarifa zako kama ulivyoziorozesha wakati wa kujiandikisha katika huduma zake, pamoja na zile unazobadilishana na watu mbalimbali.

Lengo kuu la Google kufanya hivyo ni ili kuweza kukuletea Mapendekezo Yanayokulenga moja kwa moja.

Mfano; kama umezoea kuandika email (barua pepe) kwa John na kisha ukaicopy kwa Mussa, basi kila utakapoandika email google yaweza kukupa pendekezo la kujumuisha na email ya Mussa.
Mfano mwingine ni kama unatafuta wimbo fulani kwa youtube Google inaweza pendekeza wimbo mwingine kuendana na historia inavyojionyesha kuwa wewe unapendelea nyimbo za namna gani.

Hii pia inasaidia Google kukuletea matangazo yanayokuhusu moja kwa moja. Mfano kama kipindi hiki umekuwa sana ukifuatilia habari za kazi basi usishangae ukiwa unasearch nyimbo kwa youtube Google ikakuletea tangazo la kazi.

Ni hayo tuu kwa leo, kujisomea zaidi kuhusu Sera hii na jinsi ya kujihadhari BOFYA HAPA

0 comments: